

Lugha Nyingine
Marais wa China na Msumbiji watumiana pongezi juu ya maadhimisho ya miaka 50 ya uhusiano wa kidiplomasia
Rais Xi Jinping wa China na mwenzake wa Msumbiji Daniel Chapo leo Jumatano wametumiana salamu za pongezi kusherehekea maadhimisho ya kutimia miaka 50 tangu kuanzishwa uhusiano wa kidiplomasia kati ya nchi hizo mbili.
Kwenye ujumbe wake Rais Xi amesema, katika kipindi chote cha miaka hiyo 50, bila kujali hali ya kimataifa inavyobadilika, China na Msumbiji siku zote zimekuwa zikiaminiana na kuungana mkono, na kwamba urafiki kati ya nchi mbili umezidi kuimarika.
Rais Xi ameeleza imani yake kuwa uhusiano wa pande mbili utazidi kuwa na mustakabali mzuri zaidi katika siku za baadaye ilimradi tu pande hizo mbili zitaendelea kushikilia nia ya awali ya kuanzishwa kwa uhusiano wa kidiplomasia na kusonga mbele bega kwa bega.
Naye Rais Chapo amesema, Msumbiji itaendelea kushikilia sera ya kuwepo kwa China Moja, huku ikiunga mkono juhudi zote za serikali ya China katika kufikia muungano wa taifa.
Amesema, Msumbiji inaunga mkono mapendekezo makuu ya China, na kwamba inapenda kuimarisha uhusiano wa pande mbili katika msingi wa kuheshimiana na kunufaishana, kupanua ushirikiano wa kivitendo, kulinda kwa pamoja mfumo wa pande nyingi na kuhimiza amani, usalama na ustawi wa dunia.
Ukumbi wa Kuutazama Mji wa “Kilele cha Tianjin” wa China wafunguliwa rasmi kwa umma
Kuendeleza urithi wa utamaduni usioshikika wa China - ustadi wa kutengeneza chai ya Taiping Houkui
Njia mpya za uendeshaji wa droni zaanza kutumika katika Mji wa Wuhan katikati mwa China
Shughuli za utalii za siku za lavender zahimiza maendeleo ya uchumi katika Mkoa wa Xinjiang, China
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma