

Lugha Nyingine
Ethiopia yatangaza kufungua sekta ya benki kwa benki za kigeni
Benki Kuu ya Ethiopia imetangaza kwamba, kwa mara ya kwanza, sekta ya benki nchini humo iko wazi kwa benki za kigeni na wawekezaji, ikiwaruhusu kushiriki katika biashara ya benki nchini humo kwa kuanzisha kampuni tanzu, matawi au ofisi za uwakilishi.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa Jumatano wiki hii na Benki hiyo, kuanzia siku hiyo, benki na wawekezaji wa kigeni wanaweza kutuma maombi ya leseni za benki kwa Benki Kuu ya Ethiopia.
Taarifa hiyo pia imesema Benki hiyo inatumai hatua hiyo italeta uwekezaji zaidi na ushindani kwa Ethiopia na kusaidia kuboresha kiwango cha huduma, ufanisi na ujumuishaji wa sekta ya benki nchini humo.
Bustani ya Kimataifa ya Pump Track ya Shenyang, China: Utambulisho Mpya wa Michezo Mjini
Ukumbi wa Kuutazama Mji wa “Kilele cha Tianjin” wa China wafunguliwa rasmi kwa umma
Kuendeleza urithi wa utamaduni usioshikika wa China - ustadi wa kutengeneza chai ya Taiping Houkui
Njia mpya za uendeshaji wa droni zaanza kutumika katika Mji wa Wuhan katikati mwa China
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma