Rwanda yapiga marufuku matumizi ya fedha za kigeni katika biashara ya ndani

(CRI Online) Juni 27, 2025

Rwanda imetangaza kanuni mpya kali zinazopiga marufuku matumizi ya fedha za kigeni, ikiwa ni pamoja na dola ya Marekani, katika miamala ya ndani, ikiungana na idadi inayoongezeka ya nchi za Afrika, ikiwemo Tanzania, zinazochukua hatua dhidi ya uwekezaji wa dola usio rasmi katika uchumi wao.

Benki ya Taifa ya Rwanda (NBR) ilisema mapema wiki hii kwamba itatoza faini kubwa kwa wafanyabiashara na watu binafsi wanaopanga bei, kutoa ankara, au kufanya mauzo kwa fedha za kigeni bila idhini rasmi.

Hatua hizo zinalenga kuimarisha matumizi ya faranga ya Rwanda, kuboresha ufanisi wa sera ya fedha, na kuzuia uhujumu uchumi unaosababishwa na kuenea kwa matumizi ya fedha za kigeni katika masoko ya ndani.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha