Mradi wa ukarabati wa njia ya reli inayosafiri mjini Mombasa wakamilika

(CRI Online) Septemba 18, 2025

Sherehe ya kukamilika kwa mradi wa ukarabati wa njia ya reli inayosafiri mjini Mombasa uliojengwa na kampuni ya China, imefanyika jana.

Rais wa Kenya William Ruto ameshiriki kwenye sherehe hiyo, na kusema mradi huo utatoa mchango mkubwa kwa ujenzi wa miundombinu nchini Kenya na manufaa makubwa kwa wananchi, na kuisaidia Mombasa kuwa mlango mkuu wa mabadilishano ya uchumi wa Afrika.

Mradi huo ulianza kujengwa na kampuni ya CRBC ya China mwezi Agosti mwaka 2022, na urefu wa reli hiyo umefikia kilomita 16.8.

(Wahariri wa tovuti:Shixi,Renato Lu)

Picha