Mapigano mapya nchini Sudan Kusini yasababisha raia kukimbia makazi yao

(CRI Online) Februari 11, 2026

Mapigano ya kikabila katika Jimbo la Jonglei, nchini Sudan Kusini yameongezeka na kusababisha raia waliokimbia makazi yao kuwa na mahitaji makubwa ya chakula, maji, hifadhi na huduma za afya.

Ofisi ya Kuratibu Masuala ya Kibinadamu ya Umoja wa Mataifa (OCHA) imesema jana Jumanne kuwa mapigano hayo yameongezeka katika maeneo ya kaskazini na katikati ya Jimbo la Jonglei, na kusababisha idadi kubwa ya watu kukimbia makazi yao, kuzuia usambazaji wa misaada na kufungwa kwa huduma za muhimu. Aidha, imeeleza kuwa usafiri wa barabara na mito umefungwa, na ndege za misaada ya kibinadamu zimezuiwa.

“Watu kukimbia makazi yao kunaongeza hatari ya kuenea kwa mlipuko wa kipindupindu, kesi 55 na vifo 7 vimeripotiwa ndani ya wiki katika kaunti za Ayod na Duk” OCHA imesema.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha