Wakaguzi wa mapatano ya kusitisha mapigano wataka migogoro nchini Sudan Kusini kusitishwa haraka

(CRI Online) Februari 22, 2026

Wakaguzi wa kusitisha mapigano nchini Sudan Kusini wametaka kusimamishwa haraka kwa mapigano yanayoendelea kati ya Jeshi la serikali ya Sudan Kusini (SSPDF) na kundi la upinzani la Jeshi la Ukombozi wa Watu wa Sudan.

Mwenyekiti wa Mfumo wa Ukaguzi na Uthibitishaji wa Mipango ya Usalama wa Mpito na Kusitisha Mapigano (CTSAMVM), Bw. Teshome Anagawe Ayana, amesema hali ya usalama imekuwa mbaya katika majimbo ya Upper Nile, Unity, Western Bahr el Ghazal, na Jonglei, jambo ambalo lina athari kubwa kwa utekelezaji wa sehemu ya pili ya Makubaliano ya 2018 yaliyohusiwa, inayotajwa kuhusu utatuzi wa mgogoro wa Sudan Kusini (R-ARCSS).

Amesema kwa sasa mchakato wa amani uko kwenye shinikizo kubwa, na kati ya Agosti 2025 na Januari 2026 pekee, wamerekodi ukiukaji 407 wa makubaliano ya kusitisha mapigano.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha