Lugha Nyingine
Watu zaidi ya 200 wafariki kufuatia maporomoko ya ardhi katika eneo la uchimbaji madini mashariki mwa DRC

(Picha/Xinhua)
Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) imesema, idadi ya watu waliofariki kufuatia maporomoko makubwa ya ardhi yaliyotokea Jumanne wiki hii kwenye eneo la uchimbaji madini ya coltan huko Rubaya, Jimbo la Kivu Kaskazini, mashariki mwa nchi hiyo imefikia watu zaidi ya 200 wakiwemo watoto 70.
Awali, iliripotiwa juzi Jumanne kuwa, watu 7 walikuwa wamefariki katika ajali hiyo huku wengine wakiwa hawajulikani walipo.
Taarifa hiyo ya hivi punde ya Wizara ya Madini ya DRC iliyotolewa jana Jumatano imesema kuwa maporomoko hayo yalisababishwa na mvua kubwa iliyonyesha siku hiyo, na kufukia njia kadhaa za kuingia migodini.

Kupatwa kwa mwezi kikamilifu kwashuhudiwa katika sehemu mbalimbali nchini China

"Tamasha la Maolong" la kabila la Wayilao lasherehekewa kwa ngoma ya dragoni mkoani Guizhou, China

Mji mkongwe wa Wuzhen, China wazindua shughuli mbalimbali wakati wa Mwaka Mpya wa Jadi wa China

Hong Kong Yasherehekea Mwaka Mpya wa Jadi wa Farasi wa China kwa Maonyesho ya Fataki
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma