Lugha Nyingine
Hong Kong Yasherehekea Mwaka Mpya wa Jadi wa Farasi wa China kwa Maonyesho ya Fataki
![]() |
| Maonesho ya fataki yaliyosherehekea Mwaka Mpya wa Jadi wa China yakionekana kwenye Bandari ya Victoria huko Hong Kong, Kusini mwa China, Februari 18, 2026. (Picha/Xinhua) |
Maonyesho ya fataki ya dakika 23 yalimulika Bandari ya Victoria ya Hong Kong siku ya Jumatano, ikiwa ni siku ya pili ya Mwaka wa Farasi na likizo ya Mwaka Mpya wa Jadi wa China kwa kalenda ya jadi ya China.
Katika saa mbili usiku, fataki nyingi zilizokuwa zikiiga mwendo wa farasi wanaokimbia zilifungua maonesho hayo, zikifuatiliwa na fataki zilizounda umbo la namba "8" na umbo la vipande vya dhahabu, ambavyo ni ishara ya utajiri na ufanisi. Vifijo vilitokea kutoka watu kwenye pande zote za bandari.
Suati za fataki hizo zitasimulia moyo wa Mwaka wa Farasi, alisema John Lee, Mkuu wa Mkoa wa Utawala Maalum wa Hong Kong (HKSAR), kabla ya onyesho kuanza.
"Usiku wa leo, wakati moyo wa kusonga mbele wakijaza anga, tunaona ni kwa nini Hong Kong ni mahali ambapo Mashariki hukutana na Magharibi — ambapo mila za kale na sherehe za kisasa huangaza usiku kwa pamoja," alisema Lee.
Kutokana na matarajio kwa tukio hilo kubwa, wakazi na watalii wengi walijipatia nafasi mapema jioni karibu na bandari ili kupata mandhari nzuri zaidi.
"Natumai maendeleo ya sayansi na teknolojia ya Hong Kong yanaweza kupaa juu kama fataki hizi zilivyofanya leo," alisema mjasiriamali mmoja kijana mwenye jina la ukoo Lau, aliyekuwa akitazama maonyesho hayo katika eneo la Central Ferry Piers.
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma




