Lugha Nyingine
Ushirikiano wa China na Afrika wahimiza ukuaji endelevu katika eneo la Ziwa Victoria (3)
![]() |
| Picha iliyopigwa Februari 27, 2026 ikionyesha mandhari ya Ziwa Victoria na Kisumu, Kenya. (Xinhua/Xie Jianfei) |
Yakiwa ni maziwa makubwa zaidi ya maji freshi nchini China na Afrika, mtawalia, Ziwa Poyang na Ziwa Victoria yameshuhudia ushirikiano wa kuvuka bara kwa ajili ya maendeleo endelevu na uhifadhi wa ikolojia.
Ziwa Victoria ni hifadhi kuu ya Mto Nile, na Ziwa Poyang linaungana na Mto Yangtze wa China. Maziwa yote mawili hutumika kama vyanzo muhimu vya maji, yakiunga mkono mamilioni ya watu na kutoa makazi kwa wanyamapori mbalimbali.
Katika miaka ya hivi karibuni, kwa uungaji mkono kutoka mashirika kama vile Mradi wa Kituo cha Maendeleo cha Dunia ya Kusini-Kusini na Mfuko wa Dhamana wa Umoja wa Mataifa wa Perez-Guerrero, Ziwa Poyang na Ziwa Victoria, yote mawili wajumbe wa Mtandao wa Maziwa Hai, yameungana kukabiliana na changamoto za pamoja, ikiwemo mmomonyoko wa udongo na uharibifu wa ardhi oevu.
Mkoa wa Jiangxi wa China, nyumbani kwa Ziwa Poyang, umeimarisha ushirikiano wake na Kenya, Tanzania na mataifa mengine yanayopakana na Ziwa Victoria katika miaka ya hivi karibuni.
Kwa kuchangia utaalamu wao katika usimamizi wa maziwa, mkoa huo na washirika wake wameingiza kasi mpya katika juhudi za China na Afrika kuelekea ujenzi wa mambo ya kisasa ulio rafiki kwa mazingira.
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma




