Eneo la kaboni-sifuri katika Mkoa wa Hainan laonyesha vitendo vya kijani vya China (5)

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Machi 25, 2026
Eneo la kaboni-sifuri katika Mkoa wa Hainan laonyesha vitendo vya kijani vya China
Picha iliyopigwa Machi 19, 2026 ikionyesha vifaa vya kuzalisha umeme kwa nishati ya jua kwenye paa la Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Jukwaa la Asia (BFA) na hoteli ya BFA katika eneo la kielelezo la kaboni-sifuri, Boao, Mkoa wa Hainan, kusini mwa China. (Xinhua/Yang Guanyu)

BOAO - Tangu "Eneo la Kielelezo la Kaboni Karibu-Sifuri la Boao" katika Mkoa wa Hainan, kusini mwa China libadilishwe jina Machi 2025 na kuitwa "Eneo la Kielelezo la Kaboni-Sifuri la Boao", eneo hilo limepata maendeleo makubwa katika uhifadhi wa nishati na kupunguza kaboni na limeingia kikamilifu katika hatua ya uendeshaji wa kila siku wa kaboni-sifuri.

Kwa mujibu wa data zilizopimwa, uzalishaji wa kaboni dioksidi unaohusiana na nishati kutoka kwenye majengo na miundombinu ya mji huo katika eneo hilo umeshuka kutoka tani 11,350.1 mwaka 2019 hadi tani takriban 14.6 mwaka 2025, ikiwa ni upunguzaji wa asilimia 99.9. Eneo hilo lilizalisha umeme wa kijani wa kWh milioni 29 kwa mwaka, na kukidhi mahitaji yake ya umeme ya mwaka ya takriban kWh milioni 19.4, huku kWh milioni 9.6 zilizobaki zikiingizwa kwenye gridi ya taifa.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha