COMESA yapitisha mkakati wa kuhimiza utekelezaji wa AfCFTA

(CRI Online) April 09, 2026

Soko la Pamoja la Mashariki na Kusini mwa Afrika (COMESA) limeridhia mkakati wa kusaidia nchi wanachama wake kutekeleza kwa ufanisi Eneo la Biashara Huria Barani Afrika (AfCFTA).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa Jumatano, mkakati huo umepitishwa kwenye mkutano maalumu wa tisa wa baraza la mawaziri uliofanyika Aprili 2, ambao pia umepitisha Mpango Mkakati wa Kipindi cha Kati wa COMESA kwa 2026-2030.

Taarifa hiyo imesema mkakati huo unatoa mbinu ya kimfumo inayowezesha nchi wanachama kutumia fursa za soko la bara hilo, huku zikiimarisha jukumu la COMESA la kuwa mjenzi wa Jumuiya ya Kiuchumi ya Afrika.

Mkutano huo umesisitiza tena dhamira ya COMESA katika kuhimiza mafungamano ya kikanda, na kuendeleza jukumu lake ndani ya mfumo mpana wa maendeleo ya bara.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha