Watu 22 wafariki dunia katika ajali ya boti DRC

(CRI Online) April 16, 2026

Wizara ya Uchukuzi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) imesema, watu 22 wamefariki dunia baada ya boti ya injini kupinduka alfajiri ya jumatatu kwenye Ziwa Tanganyika mashariki mwa nchi hiyo.

Kwa mujibu wa matokeo ya uchunguzi wa awali, boti hiyo iliondoka saa tisa usiku wa jumatatu kutoka bandari isiyo rasmi katika kijiji cha Kasama, karibu kilomita 18 kutoka Kalemie, mji mkuu wa mkoa wa Tanganyika, kabla ya kupinduka takriban saa kumi usiku.

Mamlaka hiyo imesema upepo mkali pamoja na mzigo kupita kiasi huenda vilisababisha ajali hiyo.

(Wahariri wa tovuti:Zhao Jian)

Picha