Waziri wa Mambo ya Nje wa Cuba akosoa vikali sera ya vikwazo ya Marekani dhidi ya Cuba katika UNGA

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Julai 09, 2026

Watu wakiendesha vyombo vya usafiri barabarani mjini Havana, mji mkuu wa Cuba, Julai 8, 2026. (Picha na Joaquin Hernandez/Xinhua)

Watu wakiendesha vyombo vya usafiri barabarani mjini Havana, mji mkuu wa Cuba, Julai 8, 2026. (Picha na Joaquin Hernandez/Xinhua)

UMOJA WA MATAIFA - Waziri wa Mambo ya Nje wa Cuba Bruno Rodriguez ameishutumu serikali ya Marekani kwa kufanya "vita vya pande nyingi, visivyo vya kawaida" dhidi ya Cuba, ambavyo amesema vimedumu kwa karibu miongo saba na "vimekuwa vya kikatili zaidi na kandamizi zaidi katika kipindi cha miezi saba iliyopita."

Akizungumza kwenye mjadala wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa (UNGA) juu ya "umuhimu wa kukomesha vikwazo vya kiuchumi, kibiashara na kifedha vilivyowekwa na Marekani dhidi ya Cuba," Rodriguez amesema vitisho vya uvamizi wa kijeshi vimekuwa vikianzishwa mara kwa mara na maafisa wakuu wa utawala wa Marekani.

Mbali na kizuizi cha kiuchumi, kibiashara na kifedha cha Marekani, amesema kwamba kuna hatua ambazo hazijawahi kushuhudiwa zenye matumizi ya mamlaka nje ya mipaka ya nchi, ambavyo vilikusudiwa kusababisha janga la kibinadamu na kudhoofisha kabisa utulivu wa nchi.

Mwanzoni mwa mjadala huo, Jeffrey Bartos, mwakilishi wa Marekani katika Umoja wa Mataifa anayeshughulikia usimamizi na mageuzi ya Umoja wa Mataifa, alipinga vikali kufanyika kwa mjadala wa pili juu ya mada hiyo, ambao tayari ulikuwa umeitishwa kama sehemu ya kazi ya mwaka ya UNGA mwezi Oktoba 2025.

Aliulaani kwa kuuelezea kuwa ni matumizi "ya kupoteza" fedha za Umoja wa Mataifa, kisha akaitisha kura ya kurekodiwa ya kuamua kufunguliwa tena kwa ajenda hiyo au la.

Kisha UNGA ilipitisha hoja hiyo ya kuendelea na mjadala huo, kwa kura 136 za kuunga mkono, 9 za kupinga na 30 za kujizuia kupiga kura.

Kwenye hotuba yake, Rodriguez amesema kwamba katika miezi iliyopita, uharibifu wa kibinadamu kwa watu wa Cuba umeongezeka, jambo ambalo limesababisha kuzorota kwa ubora wa maisha, kupungua kwa njia za kujikimu, ukomo wa uwezekano wa maendeleo binafsi, ya familia na kijamii, na ukiukwaji mkubwa, dhahiri na wa kimfumo wa haki za binadamu za watu wote "kwa kitendo cha adhabu ya pamoja."

"Serikali ya Marekani, na hasa Wizara yake ya Mambo ya Nje, inaeneza uwongo kwamba kizuizi hicho hakilengi watu wa Cuba," amesema.

"Unaweza kuwauliza watu wa Cuba kama wanateseka au la kwa sababu ya kizuizi hicho," amedai.

Kwa mujibu wa Rodriguez uharibifu wa jumla uliosababishwa na kizuizi hicho cha Marekani tangu kilipowekwa kwa mara ya kwanza unafikia dola bilioni 178.7 za Marekani kwa bei za sasa.

"Cuba ni taifa ambalo liko linatishiwa," Rodriguez amesema, akiongeza kuwa Cuba ni taifa lenye dhamira ya kutetea amani, sheria za kimataifa, ushirikiano wa pande nyingi, ukweli na haki. 

Jamaa akitembea kuipita kauli mbiu inayopinga kizuizi cha Marekani, mjini Havana, mji mkuu wa Cuba, Julai 8, 2026. (Picha na Joaquin Hernandez/Xinhua)

Jamaa akitembea kuipita kauli mbiu inayopinga kizuizi cha Marekani, mjini Havana, mji mkuu wa Cuba, Julai 8, 2026. (Picha na Joaquin Hernandez/Xinhua)

(Wahariri wa tovuti:Liu Mengxue,Zhao Jian)

Picha