Lugha Nyingine
Mashambulizi mapya ya Iran yaripotiwa Jordan, Kuwait, Bahrain, na kuibua wito wa kupunguza kupamba moto kwa mgogoro
Jordan, Kuwait na Bahrain zimeripoti mashambulizi mapya ya Iran siku ya Jumapili huku uhasama mpya kati ya Marekani na Iran ukienea katika nchi jirani, na kuibua wito wa kupunguza kupamba moto kwa mgogoro kote Mashariki ya Kati.
Shirika la Utangazaji la Jordan limesema katika habari yake iliyochapishwa kwenye mtandao wa X kwamba vikosi vya ulinzi wa anga vya Jordan vilizuia makombora matatu yaliyorushwa kutoka Iran kuelekea eneo la Jordan, huku la nne likianguka katika eneo la mbali kusini mwa Jordan bila kusababisha majeruhi au uharibifu wa vifaa.
Pia siku hiyo ya Jumapili, Jeshi la Kuwait lilisema ulinzi wa anga ulizuia makombora ya balestiki na droni za maadui kwenye anga ya nchi hiyo, wakati shambulio jingine lilipiga kituo cha kuzalisha umeme na kuondoa chumvi kwenye maji, na kusababisha moto na uharibifu mkubwa.
Mamlaka za Bahrain pia zimesema ulinzi wa anga wa nchi hiyo ulizuia mashambulizi kadhaa ya angani ya Iran.
Uhasama huo unaozidi kuongezeka umeibua wasiwasi mpya katika eneo lote na kupelekea kutolewa tena kwa wito.
Miongoni mwa waliotoa wito huo ni Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu, Nabil Fahmy, ambaye katika taarifa yake ya Jumapili ameonya juu ya matokeo mabaya ya kuongezeka kupamba moto huko kwa mgogoro kunakoendelea katika eneo hilo, akihimiza juhudi za kuepuka mzunguko mpya wa vurugu.
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma



