Lugha Nyingine
Shughuli ya 10 ya Siku za Kitaifa za Kakao na Chokoleti yafunguliwa nchini Cote d'Ivoire (2)
(Tovuti ya Gazeti la Umma) Septemba 03, 2026
Shughuli ya 10 ya Siku za Kitaifa za Kakao na Chokoleti imeanza mjini Abidjan, Cote d'Ivoire Jumanne wiki hii. Shughuli hiyo ya siku tatu inayofanyika chini ya kaulimbiu ya "Vijana na Kilimo cha Kakao cha Siku za Baadaye," inashirikisha aina mbalimbali za bidhaa za kakao na chokoleti, na inatoa jukwaa kwa majadiliano juu ya ushiriki wa vijana, usindikaji wa kakao wa ndani, uvumbuzi wa kiteknolojia na maendeleo endelevu ya sekta hiyo.
Inawaleta pamoja watu kutoka sehemu mbalimbali za sekta hiyo ya kakao, wakiwemo wale wanaojihusisha na kilimo, usindikaji, uuzaji nje wa kakao na uzalishaji wa chokoleti ili kushiriki.
Kakao ni moja ya mazao muhimu zaidi ya kibiashara ya Cote d'Ivoire na nguzo muhimu ya uchumi wake wa kilimo na mauzo ya nje.
(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Renato Lu)
Kuhusu Tovuti ya Gazeti la Umma
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma




