Kuanzia Tarehe 12, Novemba, 2021, Beijing imeanza kuandaa barabara maalum kwa ajili ya magari yanayotumiwa kwenye Michezo ya Olimpiki ya Majira ya Baridi na Michezo ya Olimpiki ya Majira ya Baridi ya Walemavu ya Beijing 2022, huku ikichora alama maalum kwenye barabara hizo.
Kuanzia asubuhi mapema ya tarehe 6, Novemba, kwenye msingi wa kuanguka theluji mjini Beijing, mashine za kutengeneza theluji zimeanza kufanya kazi kwenye Kituo cha kitaifa cha kuruka na kuteleza kwenye theluji kilichoko kwenye Uwanja wa Zhangjiakou wa Michezo ya Olimpiki ya Majira ya Baridi ya Beijing 2022, ili kufanya maandamizi ya majaribio ya michezo hivi karibuni.
Uwanja wa “BIG AIR” ya Shougang utafunguliwa jumatano wiki hii kwenye Bustani ya Shougang ya Beijing. (ChinaDaily/Gao Zehong) Jumba jipya la kipekee la kuteleza kwenye theluji la Michezo ya Olimpiki ya majira ya baridi ya Beijing 2022 litawawezesha wanamichezo kuhisi kama kufanya urukaji.
Kwa mujibu wa habari kutoka Ofisi ya Uongozi wa Ujenzi wa Miradi Mikubwa ya Beijing, ukarabati wa uwanja wa michezo wa taifa “kiota cha ndege”ambao utatumika kwa hafla za ufunguzi na ufungaji wa Michezo ya Olimpiki ya Majira ya Baridi ya Beijing 2022 na Michezo ya Olimpiki ya Walemavu ya Majira ya Baridi ya Beijing umekamilika Alhamisi ya wiki hii. Ujenzi wa kumbi na miundombinu wezeshi ya mashindano ya michezo hiyo nao umemalizika rasmi.