Mwanamichezo kutoka Madagascar Mialitiana CLERC ni mmoja wa wanamichezo sita kutoka nchi tano za Afrika walioshiriki kwenye Michezo ya Olimpiki ya Majira ya Baridi ya Beijing, na pia ni mwanamichezo wa kwanza mwanamke kuiwakilisha Madagascar kushiriki kwenye michezo hiyo. Hii ni mara yake ya pili kushiriki Michezo ya Olimpiki ya Majira ya Baridi na nafasi yake kwenye mashindano ya Women's Giant Slalom imepanda kutoka 48 mwaka 2008 hadi 41 hapa Beijing.
Kwaya ya watoto wakiimba wimbo wa Olimpiki wakati wa sherehe za ufunguzi wa Michezo ya Olimpiki ya Majira ya Baridi ya Beijing kwenye Uwanja wa Michezo wa Taifa hapa Beijing, Februari 4, 2022. (Xinhua/Cao Can) Katika usiku wa Februari 4, kwaya ya watoto 44 kutoka kaunti yenye milima mingi ya Kaskazini mwa China iliimba wimbo rasmi wa Olimpiki katika sherehe za ufunguzi wa Michezo ya Olimpiki ya Majira ya baridi ya Beijing 2022, wakivuta hisia za Dunia nzima kwa kujiamini katika macho yao na utulivu ya sauti zao.
Kwenye sherehe za ufunguzi wa Michezo ya Olimpiki ya Majira ya baridi ya Beijing, mshika bendera wa Samoa ya Marekani Nathan Crumpton hakuhofia baridi na alionekana katika mwili wake uliotiwa mafuta bila kuvaa shati, alivaa sketi ya nyasi na makubadhi. Baada ya sherehe za ufunguzi wa michezo hiyo, alipewa jina la "mshika bendera aliyeganda zaidi kwa baridi katika Michezo ya Olimpiki ya Majira ya Baridi" na watazamaji wa China na wa kigeni.
Mwanamke akiteleza kwenye theluji. (Picha inatoka IC.