人民网首页

Habari

Asubuhi ya Tarehe 19, Novemba kwa saa za huko, Rais Xi Jinping wa China amekutana na Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron katika wakati wa kuhudhuria kwenye Mkutano wa 19 wa kundi la nchi 20 (G20) huko Rio de Janeiro, Brazil. (Picha na Shen Hong/Xinhua)

Rais Xi Jinping wa China akutana na Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron

Rais Xi Jinping wa China amesema China na Ufaransa zina wajibu wa nchi kubwa wa kufanya jumuiya ya kimataifa kuwa na mshikamano ili kukabiliana na changamoto za kimataifa katika wakati ambao mabadiliko mengi mapya yanajitokeza katika mazingira ya kimataifa. Xi ameyasema hayo alipokutana na Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron katika wakati wa kufanyika kwa Mkutano wa Viongozi wa G20 huko Rio de Janeiro, Brazil.

Asubuhi ya Tarehe 19, Novemba kwa saa za huko, Rais Xi Jinping wa China amekutana na Chansela wa Ujerumani Chancellor Olaf Scholz katika wakati wa kuhudhuria kwenye Mkutano wa 19 wa kundi la nchi 20 (G20) huko Rio de Janeiro, Brazil. (Picha na Xie Huanchi/Xinhua)

Rais Xi Jinping wa China akutana na Chansela wa Ujerumani Chancellor Olaf Scholz

Rais Xi Jinping wa China amesema ushuru ulioongezeka wa Umoja wa Ulaya kwa magari ya umeme ya China unafuatiliwa duniani kote, ambapo China siku zote inasisitiza kutatua tofauti kwa njia ya mazungumzo na mashauriano, huku ikitarajiwa kuwa Ujerumani itaendelea kufanya kazi yake muhimu katika suala hili. Rais Xi ameyasema hayo kwenye mkutano wake na Chansela Olaf Scholz wa Ujerumani katika wakati wa kufanyika kwa Mkutano wa Viongozi wa G20 huko Rio de Janeiro, Brazil, akisistiza kuwa China inaiona Ulaya kama nguzo muhimu katika dunia yenye ncha nyingi, na kuongeza kuwa China imejitolea kushirikiana na Ulaya ili kukabiliana na changamoto kwa pamoja na kukuza maendeleo endelevu na thabiti ya uhusiano kati ya China na Umoja wa Ulaya.

Xi awasili Brasilia kwa ziara ya kiserikali nchini Brazil

Asubuhi ya Tarehe 19, Novemba kwa saa za huko, Rais Xi Jinping wa China amewasili Brasilia kwa ziara ya kiserikali nchini Brazil. Baada ya kuwasili uwanja wa ndege alilakiwa na Rui Costa, mkurugenzi wa ofisi ya Ikulu ya rais pamoja na maofisa wengine waandamizi wa Brazil, ambapo wasanii wanawake wa Bendi ya Batala walipiga muziki wa ngoma ulio wa furaha na uchangamfu kwa kumkaribisha.

Asubuhi ya Tarehe 18, Novemba kwa saa za huko, Rais Xi Jinping wa China amekutana na Waziri Mkuu wa Uingereza Keir Starmer katika wakati  wa kuhudhuria kwenye Mkutano wa 19 wa kundi la nchi 20 (G20) huko Rio de Janeiro, Brazil. 
(Picha na Shen Hong/Xinhua)

Rais Xi Jinping wa China akutana na Waziri Mkuu wa Uingereza Keir Starmer

Iliyopita1 2 3 4 5 6 Inayofuata