人民网首页

Picha

Gexi Wangmu (Kulia) akifahamishwa kuhusu huduma za afya za eneo husika alipomtembelea mwanakijiji mzee katika Kijiji cha Songgang cha Mji wa Maerkang, Eneo linalojiendesha la Makabila ya Watibet na Waqiang la Aba, Mkoa wa Sichuan, kusini-magharibi mwa China, Februari 18, 2025. (Xinhua/Wang Xi)

Mjumbe wa Bunge la Umma la China adumisha mawasiliano na wakazi wazee kupitia huduma za matunzo

ABA - Gexi Wangmu, ni mjumbe wa Bunge la 14 la Umma la China, anayefanya kazi kama mkurugenzi wa kituo cha matunzo ya wazee katika Mji wa Maerkang wa Mkoa wa Sichuan, Kusini Magharibi mwa China. Akiwa ni mjumbe wa bunge hilo wa "kuzaliwa baada ya miaka ya 90", Gexi alianza maisha yake ya utumishi kama mfanyakazi wa mstari wa mbele wa huduma za matunzo ya wazee, na amejitolea kwa miaka 16 katika kazi yake hiyo.

Sun Jingnan (wa pili kushoto) akizungumza na wafanyakazi wenzake katika karakana ya CRRC Tawi la Nanjing Puzhen, Mkoa wa Jiangsu wa China, mashariki, Februari 20, 2025. (Xinhua/Li Bo)

Mjumbe wa Bunge la China na mchomeleaji vyuma mstadi anayejitoa kwa mafunzo ya mafundi vijana

NANJING - Sun Jingnan amekuwa akifanya kazi kama mchomeleaji vyuma katika Kampuni ya Vifaa vya Reli ya CRRC ya China Tawi la Nanjing kwa zaidi ya miongo mitatu, na pia shahidi wa maendeleo ya haraka ya sekta ya usafiri wa reli ya China. Akiwa amekua kutoka fundi kijana hadi kuwa mtaalamu, Sun ni mshauri na mlezi kitaaluma kwa vijana wengi wenye vipaji katika sekta hiyo ya reli.

Kamati ya Kudumu ya Bunge la China yapanga mkutano wake kufanyika mwishoni mwa Februari

Zhao Leji, mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge la Umma la China, akiongoza mkutano wa 38 wa Baraza la Wenyeviti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge la 14 la Umma la China kwenye Jumba la Mikutano ya Umma la Beijing, China, Februari 17, 2025. (Xinhua/Yao Dawei) BEIJING - Kamati ya Kudumu ya Bunge la 14 la Umma la China itafanya mkutano wake wa 14 mjini Beijing Februari 24 na 25.

Iliyopita1 2 3 4