Hafla ya uzinduzi wa Mwaka wa 2026 wa Mawasiliano kati ya Watu wa China na Afrika ikifanyika kwenye makao makuu ya Umoja wa Afrika (AU) mjini Addis Ababa, mji mkuu wa Ethiopia, Januari 8, 2026. (Xinhua/Han Xu) JOHANNESBURG - Mwaka huu unatimiza miaka 70 tangu kuanzishwa kwa uhusiano wa kidiplomasia kati ya China na Afrika.
Waziri wa Mambo ya Nje wa China Wang Yi, ambaye pia ni Mjumbe wa Ofisi ya Siasa ya Kamati Kuu ya Chama cha Kikomunisti cha China (CPC), na Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika (AU) Mahmoud Ali Youssouf wakifanya kwa pamoja Mazungumzo ya tisa ya Kimkakati kati ya China na AU kwenye makao makuu ya AU mjini Addis Ababa, mji mkuu wa Ethiopia, Januari 8, 2026. (Xinhua/Han Xu) Waziri wa Mambo ya Nje wa China Wang Yi na Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika (AU) Mahmoud Ali Youssouf kwa pamoja wamefanya Mazungumzo ya 9 ya Kimkakati kati ya China na AU kwenye makao makuu ya Umoja huo mjini Addis Ababa, Ethiopia.