ZANZIBAR - Asubuhi ya Jumamosi yenye mwanga angavu huko Kombeni, nje kidogo ya Jiji la Zanzibar, Tanzania, mfanyakazi wa ulinzi mwenye umri wa miaka 71 Amin Maulid Juma alitoka kwenye Kliniki ya Sinai akiwa na hisia mpya ya unafuu na shukrani. Kwa wiki kadhaa, alikuwa amevumilia usiku mfululizo wa kukosa usingizi kutokana na maumivu ya tumbo yasiyokoma.
DAR ES SALAAM - Saluni ya kitamaduni iliyofanyika Jumapili jioni jijini Dar es Salaam, Tanzania iliwaleta pamoja wasanii kutoka China na Tanzania na kuonyesha dhahiri ubadilishanaji wa kistaarabu unaolenga kuzidisha uhusiano wa kitamaduni kati ya nchi hizo mbili. Shughuli hiyo, iliyoandaliwa na Ubalozi wa China nchini Tanzania, Kituo cha China cha Ubadilishanaji wa Kimataifa wa Kitamaduni na Kuhimiza Utalii nchini Tanzania, iliwaleta pamoja maafisa wa serikali, wasomi, wasanii, na wajumbe wa jumuiya ya Wachina nchini Tanzania.
Jumamosi, Mei 23 Tamasha la Utamaduni la Siku ya Afrika kwa Waafrika wanaoishi China lilifanyika mjini Beijing, mji mkuu wa China likivutia watu wengi kuja kujionea utajiri wa utamaduni wa Afrika na mambo mbalimbali yanayowakilisha ushirikiano na ukaribu wa muda mrefu wa kati ya China na Afrika. Katika tamasha hilo, moja ya vivutio vikubwa ilikuwa mitindo ya mavazi ya kijadi kutoka tamaduni mbalimbali za Afrika.
Tamasha la wazi la Siku ya Afrika mwaka 2026 likifanyika mjini Beijing, China, Mei 23, 2026. (Picha na People’s Daily Online) Tamasha la wazi la Siku ya Afrika mwaka 2026 kwa Waafrika wanaoishi China limefanyika mjini Beijing, China juzi Jumamosi likiwaleta pamoja wanadiplomasia wanaoziwakilisha nchi mbalimbali duniani hususani za Afrika, maofisa wa serikali ya China, wawakilishi wa mashirika ya kimataifa nchini China na watu wa pande mbili za China na Afrika kusherehekea utajiri wa kitamaduni wa Afrika.