Lugha Nyingine
Rais wa Marekani aambukizwa COVID-19
(CRI Online) Julai 22, 2022
Ikulu ya Marekani jana ilitangaza kuwa, rais wa nchi hiyo Joe Biden amethibitishwa kuambukizwa COVID-19, na alikuwa na dalili ndogo.
Msemaji wa Ikulu ya Marekani Bi. Karina Jean-Pierre amesema, rais Biden ameanza matibabu na atawekwa karantini katika Ikulu na kuendelea na kazi zake kikamilifu.
Habari zinasema, rais Biden amepata dozi kamili za chanjo ya COVID-19 na dozi mbili za nyongeza.
(Wahariri wa tovuti:Zhou Linjia,Zhao Jian)
Kuhusu Tovuti ya Gazeti la Umma
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma