Reli ya Mwendokasi ya HSR nchini Indonesia yahudumia abiria zaidi ya 700,000 tangu ianze kufanya kazi kibiashara

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Desemba 18, 2023
Reli ya Mwendokasi ya HSR nchini Indonesia yahudumia abiria zaidi ya 700,000 tangu ianze kufanya kazi kibiashara
Abiria wakijipiga picha ya selfie pamoja na mfano wa treni ya mwendokasi inayotumia nishati ya umeme (EMU) ya reli ya mwendokasi ya Jakarta-Bandung katika Stesheni ya Halim mjini Jakarta, Indonesia, Desemba 17, 2023. (Xinhua/Xu Qin)

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kampuni ya PT Kereta Cepat Indonesia-China (KCIC), ambayo ni kampuni ya ubia kati ya kampuni zinazomilikiwa na serikali ya Indonesia na China zilizojenga na kuendesha reli ya mwendo kasi ya Jakarta-Bandung (HSR) nchini Indonesia, reli hiyo ya mwendokasi imeshahudumia abiria zaidi ya 700,000 tangu ilipoanza kufanya kazi rasmi kibiashara Oktoba 17 mwaka huu.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha