

Lugha Nyingine
China yarusha satalaiti mpya za kuhisi kwa mbali kwenda anga ya juu
TAIYUAN – China imerusha seti ya satalaiti za kuhisi kwa mbali kwenda anga ya juu kutoka Kituo cha Kurushia Satalaiti cha Taiyuan katika Mkoa wa Shanxi, kaskazini mwa China siku ya Jumapili.
Zikiwa zimerushwa majira ya saa 3:27 usiku (kwa saa za Beijing) ndani ya roketi ya Long March-6 illiyorekebishwa, satalaiti hizo za Yaogan-40 02 zimeingia kwa mafanikio kwenye obiti iliyopangwa, kampuni mrushaji imeeleza.
Kampuni hiyo imeeleza kuwa, satalaiti hizo zitatumika kufanya ukaguzi na ufuatiliaji wa mazingira ya sumaku-umeme na majaribio ya teknolojia husika.
Urushaji huo wa jana Jumapili ni safari ya 574 kufanywa na mfululizo wa roketi ya Long March, kituo hicho kimeeleza.
Upandaji mahindi waingia kipindi cha kilele katika Mkoa wa Mongolia ya Ndani, China
UNESCO latoa wito upya wa kuimarishwa ulinzi wa maeneo ya urithi ya Afrika
Maonyesho ya Kimataifa ya Baiskeli ya China 2025 yaanza Shanghai
Shaolin Kungfu, chombo muhimu cha mawasiliano ya Utamaduni wa China na ulimwengu wa nje
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma