Siku ya Kimataifa ya Wauguzi yaadhimishwa katika Mkoa wa Mongolia ya Ndani, China

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Mei 13, 2025
Siku ya Kimataifa ya Wauguzi yaadhimishwa katika Mkoa wa Mongolia ya Ndani, China
Muuguzi akimtundikia dripu mgonjwa katika Hospitali ya Kimongolia ya Kimataifa ya Mongolia ya Ndani mjini Hohhot, Mkoa unaojiendesha wa Mongolia ya Ndani, Kaskazini mwa China, Mei 12, 2025. (Xinhua/Ma Jinrui)

Wauguzi wa Hospitali ya Kimongolia ya Kimataifa ya Mongolia ya Ndani mjini Hohhot, Mkoa unaojiendesha wa Mongolia ya Ndani, Kaskazini mwa China wamekuwa na shughuli nyingi za kuwahudumia wagonjwa kwenye vituo vyao vya kazi katika Siku ya Kimataifa ya Wauguzi ambayo huadhimishwa kote duniani kila ifikapo Mei 12 ya kila mwaka.

Kwa kupitia kazi ya kuunganisha matibabu za kijadi za Kimongolia kama vile kutumia chai, divai na moxibustion na mbinu za kisasa za uuguzi, wauguzi hao wanatoa huduma kwa wagonjwa ambazo zinaonesha umaalum wa matibabu ya kikabila.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha