

Lugha Nyingine
Trump asema mazungumzo ya simu na Putin "yamekwenda vizuri sana"
LOS ANGELES - Rais Donald Trump wa Marekani katika ujumbe aliouchapisha kwenye mtandao wa kijamii baada ya mazungumzo ya saa mbili ya simu kuhusu vita vya Ukraine na mwenzake wa Russia Vladimir Putin amesema mazungumzo hayo "yamekwenda vizuri sana", akisema Russia na Ukraine zitaanzisha mazungumzo ya upatanishi ambayo masharti yanaweza tu kuwekwa na pande hizo mbili zenyewe.
"Russia na Ukraine mara moja zitaanza mazungumzo ya upatanishi kuhusu Kusimamisha mapigano na, muhimu zaidi, MWISHO wa Vita," Trump ameandika, akiongeza kuwa "masharti ya hilo yatajadiliwa kati ya pande hizo mbili, kwani inawezekana tu, kwa sababu wanajua mambo halisi ya mazungumzo ya upatanishi ambayo hakuna mwingine anaweza kujua."
Trump amesema kuwa Russia inataka "kufanya BIASHARA kubwa na Marekani" wakati hali mbaya ya sasa ikiwa imekwisha na akaelezea imani yake kuwa Ukraine inaweza kunufaika kutoka kwenye biashara vilevile.
"Kuna fursa kubwa kwa Russia kutengeneza idadi kubwa ya ajira na utajiri. Uwezekano wake kifursa ni USIO NA KIKOMO. Vile vile, Ukraine inaweza kuwa mnufaika mkubwa wa Biashara, katika mchakato wa kujenga upya Nchi yake," ujumbe huo unasomeka.
Trump pia amesema ameambia Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky na viongozi wengine kuhusu mawasiliano hayo ya simu, akiwemo Rais wa Kamisheni ya Ulaya Ursula von der Leyen, Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron, Waziri Mkuu wa Italia Giorgia Meloni, Chansela wa Ujerumani Friedrich Merz na Rais wa Finland Alexander Stubb.
Miti ya jacaranda katika mchanuo wa maua yavutia watalii mjini Kunming, China
Upandaji mahindi waingia kipindi cha kilele katika Mkoa wa Mongolia ya Ndani, China
UNESCO latoa wito upya wa kuimarishwa ulinzi wa maeneo ya urithi ya Afrika
Maonyesho ya Kimataifa ya Baiskeli ya China 2025 yaanza Shanghai
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma