Bw. Wang Yi akutana na mawaziri wa mambo ya nje wa nchi za Afrika

(CRI Online) Juni 11, 2025

Waziri wa Mambo ya Nje wa China Bw. Wang Yi jana Jumanne kwa nyakati tofauti alikutana na baadhi ya wenzake wa nchi za Afrika waliokuja China kuhudhuria Mkutano wa Ngazi ya Mawaziri wa Waratibu kuhusu Utekelezaji wa Hatua Fuatiliaji za Baraza la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) mjini Changsha, mkoani Hunan.

Mawaziri hao wa mambo ya nje ni pamoja na Bw. Musalia Mudavadi wa Kenya, Bw. Yassine Fall wa Senegal, Bw. Mahmoud Thabit Kombo wa Tanzania, Bw. Selma Ashipala-Musavyi wa Namibia, Bw. Phenyo Butale wa Botswana na Bw. Tete Antonio wa Angola.

Kwenye mikutano hiyo na mawaziri hao wa Afrika, Bw. Wang Yi amesema mkutano huo wa mawaziri ni mkusanyiko wa China na nchi za Afrika, na kwamba utaimarisha mshikamano wa nchi hizo katika Dunia ya Kusini.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha