

Lugha Nyingine
Rais wa Guinea-Bissau azindua barabara kuu iliyojengwa kwa ufadhili wa China
Rais wa Guinea-Bissau Umaro Sissoco Embalo jana Jumatatu aliongoza hafla ya uzinduzi wa barabara kuu inayounganisha mji mkuu wa nchi hiyo, Bissau na kitongoji chake cha Safim, ikiwa na umbali wa kilomita 8.2.
Barabara hiyo kuu imejengwa na kampuni ya barabara na madaraja ya Longjian ya China, na kufadhiliwa kikamilifu na serikali ya China kwa gharama ya dola za Kimarekani milioni 30.
Kwenye hafla hiyo ya uzinduzi, Rais Embalo amesema kuwa barabara hiyo ni alama ya urafiki mkubwa, mshikamano, na ushirikiano unaoendelea kati ya Guinea-Bissau na China.
Balozi wa China nchini Guinea-Bissau Yang Renhuo amesisitiza dhamira ya China ya kuendelea kuiunga mkono Guinea-Bissau katika miradi yake ya maendeleo.
Wajenzi waendelea kujenga daraja refu zaidi duniani katika Mkoa wa Guizhou wa China
Majira ya kuvuna mazao ya mpunga yawadia katika Mkoa wa Hainan, Kusini mwa China
Migodi iliyotelekezwa yageuzwa kuwa vivutio vya kitalii katika Mkoa wa Shandong, China
LEGOLAND Shanghai Resort kuanza shughuli za majaribio kabla ya kufunguliwa Julai
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma