

Lugha Nyingine
Zambia yasitisha majaribio ya chanjo dhidi ya VVU baada ya Marekani kuondoa ufadhili
Vyombo vya habari vya Zambia vimeripoti Alhamisi kuwa mamlaka ya afya ya Zambia imesitisha majaribio ya kimatibabu yaliyopangwa ya chanjo dhidi ya VVU baada ya Marekani kuondoa ufadhili.
Mwezi Januari, Mamlaka ya Taifa ya Usalama wa Kibiolojia ya Zambia iliidhinisha majaribio ya kimatibabu ya chanjo hiyo dhidi ya VVU kufanyika katika Kituo cha Utafiti wa Afya ya Familia cha Zambia (CFHRZ), chini ya ufadhili kutoka Shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Marekani (USAID).
Hata hivyo, mkurugenzi wa mradi katika CFHRZ William Kilembe amethibitisha kuwa majaribio hayo yamesitishwa mwezi Februari kutokana na ukosefu wa fedha kutoka USAID.
Ameongeza kuwa shughuli zote zimesitishwa, zikiwemo za utafiti na mpango wa chanjo, na kazi nyingine husika.
Njia mpya za uendeshaji wa droni zaanza kutumika katika Mji wa Wuhan katikati mwa China
Shughuli za utalii za siku za lavender zahimiza maendeleo ya uchumi katika Mkoa wa Xinjiang, China
Wajenzi waendelea kujenga daraja refu zaidi duniani katika Mkoa wa Guizhou wa China
Majira ya kuvuna mazao ya mpunga yawadia katika Mkoa wa Hainan, Kusini mwa China
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma