China yalaani vikali mashambulizi ya Marekani dhidi ya Iran

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Juni 23, 2025

BEIJING - China inalaani vikali mashambulizi ya Marekani dhidi ya Iran na upigaji mabomu wake dhidi ya vituo vya nyuklia vilivyo chini ya uangalizi wa Shirika la Kimataifa la Nishati ya Atomiki, msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya China amesema jana Jumapili alipotakiwa kutoa maoni yake kuhusu Rais wa Marekani Donald Trump kutangaza kwamba Marekani imefanya mashambulizi dhidi ya vituo vitatu vya nyuklia nchini Iran.

Msemaji huyo amesema, "Hatua za Marekani zimekiuka vibaya nia na kanuni za Katiba ya Umoja wa Mataifa na sheria za kimataifa, na kuifanya hali ya Mashariki ya Kati izidi kuwa mbaya," China inatoa wito kwa pande husika, hasa Israel, kusimamisha vita haraka iwezekanavyo, kuhakikisha usalama wa raia, na kuanza mazungumzo na majadiliano.

Msemaji huyo amesema China inapenda kushirikiana na jumuiya ya kimataifa katika kufanya juhudi pamoja na kulinda haki, na kufanya jitahidi zaidi kwa ajili ya kurejesha amani na utulivu katika Mashariki ya Kati. 

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha