

Lugha Nyingine
Vikosi vya Somalia na AU vyachukua tena udhibiti wa maeneo ya kimkakati kutoka kundi la Al-Shabab
Ujumbe wa Umoja wa Afrika wa Kuleta Uungaji Mkono na Utulivu nchini Somalia (AUSSOM) umesema, vikosi vyake kwa kushirikiana na jeshi la Somalia (SNAF) vimechukua tena udhibiti wa maeneo ya kimkakati ya Sabiid na Anole kutoka kundi la Al-Shabab.
AUSSOM imesema kwenye taarifa iliyotolewa jana Jumapili mjini Mogadishu kuwa, hatua hiyo inafuatia operesheni ya pamoja ya siku tatu iliyoitwa “Dhoruba ya Kimya” (Silent Storm), ambayo inalenga kukomboa maeneo yanayoshikiliwa na kundi la Al-Shabab katika Jimbo la Lower Shabelle nchini humo.
Kamanda wa sekta ya kwanza ya AUSSOM Bw. Joseph Ssemwanga amesema, operesheni hiyo itaendelea katika majimbo ya Middle Shabelle, hadi matishio ya kundi la Al-Shabab yatakapokuwa yameondolewa kikamilifu.
Njia mpya za uendeshaji wa droni zaanza kutumika katika Mji wa Wuhan katikati mwa China
Shughuli za utalii za siku za lavender zahimiza maendeleo ya uchumi katika Mkoa wa Xinjiang, China
Wajenzi waendelea kujenga daraja refu zaidi duniani katika Mkoa wa Guizhou wa China
Majira ya kuvuna mazao ya mpunga yawadia katika Mkoa wa Hainan, Kusini mwa China
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma