

Lugha Nyingine
Timu ya madaktari wa China yatoa huduma za afya bila malipo kwa watoto yatima zaidi ya 200 wa Zanzibar
Kundi la 34 la Timu ya ya madaktari wa China waliopo Tanzania Zanzibar limetoa huduma ya afya bila malipo kwa watoto yatima zaidi ya 200 na wafanyakazi katika kituo cha watoto yatima cha visiwani humo.
Madaktari wa China kutoka idara mbalimbali, ikiwemo upasuaji, magonjwa ya wanawake na meno, wamefanya uchunguzi wa kina wa mwili kwa watoto na wafanyakazi katika kituo hicho, na kutoa maelekezo kwa wafanyakazi wa kituo hicho kuhusu huduma za mwendelezo na utaratibu wa matibabu kwa wale waliokutwa na magonjwa.
Kiongozi wa timu hiyo Chen Wei amesema, kupitia shughuli hiyo, wanatarajia si tu kulinda afya ya watoto na wafanyakazi hao, bali pia kuwashawishi kukabiliana na maisha kwa ujasiri na kutimiza ndoto zao.
Naye ofisa ushirikiano wa sekta ya afya katika Wizara ya Afya Zanzibar, Mariam Khalfan amesema madaktari wa China wamerejesha matumaini kwa watoto yatima wa Zanzibar na kupanda mbegu ya urafiki ambayo inaendelea kuimarisha uhusiano kati ya pande hizo mbili.
Njia mpya za uendeshaji wa droni zaanza kutumika katika Mji wa Wuhan katikati mwa China
Shughuli za utalii za siku za lavender zahimiza maendeleo ya uchumi katika Mkoa wa Xinjiang, China
Wajenzi waendelea kujenga daraja refu zaidi duniani katika Mkoa wa Guizhou wa China
Majira ya kuvuna mazao ya mpunga yawadia katika Mkoa wa Hainan, Kusini mwa China
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma