

Lugha Nyingine
Tanzania mwenyeji mkutano wa mabaraza ya vyombo vya habari Afrika
Wakati jitihada mbalimbali za kuimarisha uhuru wa vyombo vya habari nchini Tanzania zikiendelea kufanyika, nchi hiyo itakuwa mwenyeji wa mkutano wa kimataifa wa mabaraza ya vyombo vya habari barani Afrika uliopangwa kufanyika Julai 14 hadi 17, 2025 jijini Arusha.
Akizungumza na waandishi wa habari juu ya mkutano huo, Mtendaji Mkuu wa Baraza la Vyombo vya Habari Tanzania (MCT), Ernest Sungura amesema mbali na mkutano huo, MCT pia iko mbioni kufanya utafiti kuangazia mabadiliko ya sheria na uwepo wa bodi ya ithibati, maana na athari zake katika tasnia ya habari.
Sungura amesema baraza hilo linaandaa mkutano huo kwa mara ya kwanza kwa kushirikiana na Mtandao wa Mabaraza Huru ya Vyombo vya Habari Afrika, Umoja wa Mabaraza ya Vyombo vya Habari ya Afrika Mashariki na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ya Tanzania kama mshirika mahsusi.
Kwa mujibu wa takwimu za Kielezo cha Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani (World Press Freedom Index) kinachoratibiwa na Taasisi ya Reporters Without Borders (RWB) Tanzania sasa inashika nafasi ya 97 katika nchi zinazozingatia uhuru wa vyombo vya habari ikiwa imepanda kutoka nafasi ya 142 mwaka 2023.
Njia mpya za uendeshaji wa droni zaanza kutumika katika Mji wa Wuhan katikati mwa China
Shughuli za utalii za siku za lavender zahimiza maendeleo ya uchumi katika Mkoa wa Xinjiang, China
Wajenzi waendelea kujenga daraja refu zaidi duniani katika Mkoa wa Guizhou wa China
Majira ya kuvuna mazao ya mpunga yawadia katika Mkoa wa Hainan, Kusini mwa China
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma