

Lugha Nyingine
Rwanda yakaribisha tangazo la amani kati ya DRC na waasi wa M23
Rwanda imeeleza kukaribisha kusainiwa kwa tangazo la kanuni kati ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na kundi la waasi la Vuguvugu la Machi 23 (M23) mjini Doha, Qatar, likilenga kumaliza mgogoro wa mashariki mwa DRC.
Kufuatia miezi kadhaa ya mazungumzo ya upatanishi yaliyosimamiwa na Qatar, tangazo hilo linaeleza muundo wa kanuni za kimsingi zilizokubaliwa na pande mbili, na kuweka msingi wa mazungumzo endelevu kuelekea makubaliano ya amani ya kina.
Katika taarifa iliyotolewa na wizara ya mambo ya nje ya Rwanda juzi Jumamosi, Rwanda pia imepongeza juhudi za upatanishi za Qatar, ikibainisha kuwa ni mwendelezo wa kazi ya Umoja wa Afrika na mipango mingine ya kikanda.
Imesisitiza kuwa itaendelea kuunga mkono na kuchangia amani na maendeleo katika eneo la Maziwa Makuu.
Wilaya ya Xuan’en yahimiza utalii wa usiku kando ya Mto Gongshui Katikati mwa China
Eneo la mtaa mkongwe lawa na ustawi kwa uvumbuzi wa kitamaduni na utalii mkoani Jiangxi, China
Mji wa Tianjin, China waharakisha ufungamanishaji wa uchumi wa kidijitali na uchumi halisi
Ardhioevu yalinda spishi za ndege kutoka kwenye uwanda hadi mijini
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma