Lugha Nyingine
Madaktari wa China wahimiza uelewa wa tiba ya akyupancha na malaria katika chuo kikuu cha Zanzibar, Tanzania
Kundi la 35 la Timu ya Madaktari wa China visiwani Zanzibar, Tanzania limefanya zoezi la uhamasishaji wa kiutamaduni juu ya tiba ya akyupancha na kutoa muhadhara kuhusu kinga dhidi ya malaria katika Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA), ikiwashirikisha wanafunzi kupitia mazungumzo ya kimaarifa na vitendo.
Ikiwa imealikwa na SUZA, timu hiyo iliandaa tukio hilo siku ya Jumamosi ikichanganya elimu ya afya ya umma na uhamasishaji juu ya Matibabu ya Jadi ya Kichina (TCM).
Mtaalamu wa afya ya umma wa timu hiyo, Liu Yaobao amesema zoezi hilo lilivutia ushiriki mkubwa wa wanafunzi na wahadhiri, na kuweka mazingira shirikishi na ya shauku. Pia ameelezea hali ya sasa ya malaria Zanzibar kwa kutumia lugha dhihirishi na nyenzo za kuonesha.
Mohammed Makame Haji, makamu mkuu wa Chuo Kikuu cha SUZA, amesema tukio hilo limeonesha mvuto wa kipekee wa tiba ya akyupancha huku likitoa maarifa ya kivitendo ya afya. Aidha amesema ana matumaini kwamba shughuli kama hiyo zitafanyika zaidi katika siku zijazo.
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma



