Rais wa Zanzibar asifu miradi ya miundombinu inayoungwa mkono na China

(CRI Online) Januari 07, 2026

Rais wa Zanzibar ya Tanzania Dk. Hussein Mwinyi ameisifu China kwa uungaji mkono wake katika maendeleo ya miundombinu ya Zanzibar, akisema miradi muhimu inayotekelezwa na kampuni za China visiwani Zanzibar inaendelea vizuri na itasaidia kuboresha hali ya usafiri katika visiwa hivyo.

Rais Mwinyi ameyasema hayo jana Jumanne alipohudhuria hafla ya uzinduzi wa barabara ya juu ya kwanza ya daraja iliyojengwa na shirika la uhandisi wa ujenzi la China (CCECC), akisema timu ya mradi huo imeshinda changamoto za ujenzi na kutoa michango chanya katika maendeleo ya miundombinu ya Zanzibar.

Amesema mradi huo pamoja na mradi wa barabara ya pwani ya kusini mwa Zanzibar yenye urefu wa kilomita 2.2, ina umuhimu mkubwa katika kuimarisha taswira ya mji na kuboresha maisha ya watu.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha