Lugha Nyingine
TAZARA kuanza tena huduma za treni za abiria kati ya Tanzania na Zambia
Mamlaka ya Reli ya Tanzania-Zambia (TAZARA) imetangaza kuwa huduma za treni za abiria za kuvuka mpaka kati ya Tanzania na Zambia zitaanza tena Februari 10.
Taarifa iliyotolewa Jumanne na TAZARA imesema hatua hiyo inalenga kurejesha ushirikiano thabiti wa reli kati ya nchi hizo mbili, kufuatia kusitishwa kwa huduma za abiria za kuvuka mpaka mwezi Juni 2024 kutokana na changamoto za kiufundi na kiutendaji.
Taarifa hiyo pia imesema hatua hiyo pia inasisitiza jukumu la awali la kuanzishwa kwa TAZARA la kuhimiza usafirishaji, biashara, utalii na mabadilishano ya kati ya watu ya kikanda.
Mkurugenzi Mkuu wa TAZARA Bw. Bruno Ching'andu amesema kuanza tena kwa huduma hiyo kunahusu kurejesha imani katika usafiri wa reli wa kuvuka mpaka kupitia huduma bora ya usafirishaji wa abiria iliyo makini, endelevu, na inayoaminika.
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma



