Lugha Nyingine
Ubalozi wa China nchini Afrika Kusini Wazindua Mwaka 2026 wa Mawasiliano kati ya Watu wa China na Afrika
Ubalozi wa China nchini Afrika Kusini jana Jumatatu mjini Pretoria ulifanya hafla ya kusherehekea uzinduzi wa Mwaka 2026 wa Mawasiliano kati ya Watu wa China na Afrika.
Mwaka huu pia ni maadhimisho ya miaka 70 tangu kuanzishwa kwa uhusiano wa kidiplomasia kati ya China na nchi za Afrika.
Akizungumza kwenye hafla hiyo, Balozi wa China nchini Afrika Kusini Wu Peng amesema katika miongo saba iliyopita, chini ya mwongozo wa pamoja wa viongozi kutoka pande zote mbili, mawasiliano ya kiutamaduni na ya kati ya watu wa China na Afrika yameendelea kupanuka na kuzaa matunda.
Akibainisha kuwa dunia inapitia mabadiliko makubwa ambayo hayajawahi kuonekana katika miaka 100 iliyopita, Balozi Wu amesema China na Afrika zinahitaji kudumisha haki na usawa, kuimarisha mshikamano na kusaidiana, na kuboresha mabadilishano na ushirikiano kuliko hapo awali.
Naye Naibu Waziri wa Wanawake, Vijana, na Watu Wenye Ulemavu wa Afrika Kusini, Mmapaseka Steve Letsike, amesema Afrika Kusini na China zinafurahia uhusiano imara na wa kihistoria wa kirafiki zikiwa ni washirika wa karibu wa ushirikiano wa kimataifa katika nyanja za kisiasa, kiuchumi, kijamii, kiufundi na mfumo wa pande nyingi.
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma



