Lugha Nyingine
Kuielewa China | Je, China itadhibiti kila kitu?
Uundaji wa kisayansi na utekelezaji endelevu wa mipango ya miaka mitano ni njia muhimu ambayo kwayo Chama cha Kikomunisti cha China kinaitawala nchi, na dirisha muhimu kwa jumuiya ya kimataifa kuielewa vyema zaidi safari ya China ya kuelekea mambo ya kisasa yenye umaalumu wa China.
People's Daily Online imezindua kipindi kipya cha "Kuielewa China," kinachofuatilia Mpango wa 15 wa Miaka Mitano (2026-2030) wa China. Kipindi hiki kinachambua kwa kina mipango ya maendeleo ya China, fursa zinazojitokeza, na mbinu zake za utawala, ili kufafanua dhana potofu na kuongeza uelewa na utambuzi wa pande zote mbili.
Kipindi hiki cha "Kuielewa China" kinawasilisha mazungumzo kati ya Ji Deqiang, Profesa na Mkurugenzi wa Kituo cha Kitaifa cha Masomo ya Uvumbuzi wa Mawasiliano katika Chuo Kikuu cha Mawasiliano cha China, na Martin Lockett, Profesa wa Usimamizi wa Kimkakati katika Shule ya Biashara ya Chuo Kikuu cha Nottingham Tawi la China. Mazungumzo yao yanachambua kwa kina jinsi juhudi za China za kuharakisha kujitegemea kwa kiwango cha juu katika sayansi na teknolojia zitakavyoathiri ukuaji wake wa uchumi na uvumbuzi duniani.
Je, China itadhibiti kila kitu? Akizungumzia wasiwasi wa nje kuhusu maendeleo ya teknolojia ya China, Lockett anasema kuwa wasiwasi kama huo, kwa namna fulani, unatokana na mafanikio ya China katika viwanda na sekta nyingine. Anasisitiza kwamba kile kinachoitwa nadharia ya "tishio la China" imetiwa chumvi, akiongeza kuwa ama kwa misingi ya mitazamo iliyopitwa na wakati, au kutokana na kutoelewana.
Kwa mtazamo wa Lockett, juhudi za China za kuimarisha kujitegemea kwa kiwango cha juu katika sayansi na teknolojia ni mwitikio wa mazingira ya nje yasiyo na uhakika, na pia ni hatua ya kujichukulia jukumu kwa hiari. Anatumia dhana ya "uwezo pacha" (ambidexterity) katika utafiti wa biashara ya kimataifa na anasema: "Kujiendeleza na kujitegemea katika sayansi na teknolojia kunamaanisha, kwa upande mmoja, kuwa na uwezo wa kumiliki teknolojia muhimu, bidhaa za msingi na huduma muhimu, ili mfumo uweze kuendelea bila kutegemea kabisa nchi moja au nchi kadhaa. Lakini pia lazima tutambue kwamba, uchumi wa dunia wenye ufanisi hauwezi kuwepo bila ushirikiano wenye tija. Changamoto halisi ni kuweza kuyatekeleza mambo haya mawili kwa wakati mmoja."
Katika mazungumzo hayo, Ji anasema kwamba China haina nia ya kudhibiti kila kitu. "China ina hisia ya uwajibikaji," Ji anasema, akieleza kuwa wajibu huu unaonekana si tu katika kuendeleza uchumi wa ndani unaotegemea teknolojia za hali ya juu, lakini pia katika kusaidia nchi zinazoendelea kukuza uchumi wao wa kidijitali na kunufaika na manufaa ya soko. Ameongeza kuwa, kwa nchi kubwa kama China, ni muhimu kumiliki uwezo muhimu katika teknolojia za msingi ili kulinda usalama wa kiteknolojia na kupunguza hatari za viwanda, lakini kujitegemea katika sayansi na teknolojia hakumaanishi kujifungia au kujitenga.
"Katika masuala mengi ya soko, naamini China ina nia ya dhati ya kuendeleza ushirikiano wa kimataifa," Ji anaongeza. Anasisitiza kwamba kuharakishwa kwa kujitegemea kwa kiwango cha juu katika sayansi na teknolojia si tu matokeo ya mchakato wa kihistoria, bali pia ni msingi muhimu wa kujenga ushirikiano wa kimataifa wenye sifa bora.
Wageni wote wawili wameonyesha kwa mifano halisi kuwa maendeleo ya sayansi na teknolojia ya China yanaenda sambamba na ufunguaji mlango. Kuanzia Mradi wa Uzalisha wa Umeme kwa Upepo wa De Aar nchini Afrika Kusini, ambao unasaidia kupunguza uhaba wa nishati, hadi Mfumo wa Urambazaji wa Satelaiti wa BeiDou unaochangia dunia; kutoka ushirikiano wa kimataifa katika kituo cha anga ya juu cha China hadi ushirikiano kati ya China na nchi nyingine katika sekta ya magari ya kisasa, mifano hiyo inaonyesha kwa kutosha kwamba China inasisitiza kujitegemea katika sayansi na teknolojia, huku ikiendelea kuwa na mwelekeo thabiti katika kufungua mlango na kuendeleza ushirikiano wa kimataifa.
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma



