Wanasayansi wa China watambua mabadiliko muhimu ya jeni za virusi vya Ebola

(CRI Online) Januari 29, 2026

Mhudumu wa afya akiua vijidudu kwa kunyunyuzia dawa kwenye kituo cha matibabu ya Ebola katika eneo maalum la afya la Bulape, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Oktoba 17, 2025. (Shirika la Afya Duniani/kupitia Xinhua)

Mhudumu wa afya akiua vijidudu kwa kunyunyuzia dawa kwenye kituo cha matibabu ya Ebola katika eneo maalum la afya la Bulape, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Oktoba 17, 2025. (Shirika la Afya Duniani/kupitia Xinhua)

Watafiti wa China wametambua mabadiliko muhimu katika jeni za virusi vya Ebola ambayo yameongeza kwa kiasi kikubwa uwezo wake wa kuambukiza wakati wa mlipuko mkubwa, na kutoa maarifa mapya kwa ajili ya ufuatiliaji wa janga na utengezaji wa dawa.

Utafiti huo kuhusu mabadiliko ya jeni za virusi vya ubora, uliochapishwa kwenye Jarida la Cell, umefanywa na timu iliyoongozwa na Profesa Qian Jun kutoka Chuo Kikuu cha Sun Yat-sen kwa ushirikiano na watafiti kutoka hospitali mbalimbali za China.

"Matokeo haya si tu kwamba yanaweza kuonya juu ya mabadiliko katika hatari ya maambukizi lakini pia kutathmini kwa ufanisi uwezo wa dawa na chanjo zilizopo, ikituongoza kurekebisha mikakati ya udhibiti wa kabla" alisema Qian.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha