Lugha Nyingine
Polisi watatu wajeruhiwa katika mlipuko wa IED mpakani mwa Kenya
(CRI Online) Februari 24, 2026
Jeshi la Polisi nchini Kenya limethibitisha kuwa polisi watatu wamejeruhiwa kwenye shambulizi la bomu la kutengenezwa kienyeji (IED) katika eneo la Harbole kaskazini mashariki mwa Kenya, karibu na mpaka na Somalia.
Jeshi hilo limesema katika ripoti yake ya usalama jana Jumatatu kwamba polisi waliojeruhiwa wamepelekwa katika kituo cha afya cha karibu ili kupata huduma ya kwanza wakati wakisubiri ndege ya kuwasafirisha hadi Nairobi kwa matibabu maalum.
Mashirika ya usalama yameongeza operesheni katika eneo hilo huku uchunguzi kuhusu shambulizi hilo ukiendelea. Eneo hilo la mpakani linachukuliwa kuwa kitovu cha makundi ya wanamgambo wanaovuka kutoka nchi jirani ya Somalia.
(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Renato Lu)
Kuhusu Tovuti ya Gazeti la Umma
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma



