Lugha Nyingine
Kundi jipya la mabaki ya askari wahanga wa China katika Vita vya Korea kurudishwa leo Jumatano (4)
BEIJING – Wizara ya Mambo ya Wanajeshi waliostaafu ya China imesema, Mabaki ya askari wahanga 12 wa Jeshi la Kujitolea la Watu wa China (CPV) waliouawa katika Vita vya Kupinga Uchokozi wa Marekani na Kuisaidia Korea (1950-1953) yatarudishwa China kutoka Korea Kusini leo Jumatano.
Ndege kubwa ya usafirishaji ya Y-20B ya Kikosi cha Anga cha Jeshi la Ukombozi wa Umma la China itawabeba mashujaa hao waliofariki hadi Shenyang, mji mkuu wa Mkoa wa Liaoning, kaskazini mashariki mwa China, ambapo ni maskani ya makaburi ya mashujaa wa CPV.
Hii ni mara ya kwanza kwa ndege hiyo ya Y-20B kubeba jukumu hilo la kurudisha mabaki ya mashujaa hao nyumbani. Baada ya kuingia tena katika anga ya China, ndege hiyo itasindikizwa na ndege nne za kivita za J-20.
Hii itakuwa mara ya 13 kurudishwa kwa mabaki ya CPV kufuatia makubaliano ya makabidhiano kati ya nchi hizo mbili. Tangu 2014, mabaki ya askari 1,011 yamesharudishwa nchini China kutoka Korea Kusini, wizara hiyo imesema.
China imeongeza juhudi za kutambua mabaki ya wahanga hao wa CPV, ikiwa ni pamoja na kuundwa kwa kanzidata ya DNA kwa ajili ya wahanga hao na jamaa zao, na kutoa uungaji mkono thabiti wa kiufundi na data ili kusaidia familia zaidi kuwapata wapendwa wao wasiojulikana waliko.
China ilituma wanajeshi milioni 2.9 wa CPV kuisaidia Jamhuri ya Watu ya Kidemokrasia ya Korea wakati wa vita, ambapo miongoni mwao zaidi ya 360,000 waliuawa au kujeruhiwa katika vita.

Ndege wa Kwarara waingia msimu wa kuzaliana huko Shaanxi, China

Eneo la kaboni-sifuri katika Mkoa wa Hainan laonyesha vitendo vya kijani vya China

Vifaa vya kisasa vya usafi vyatoa huduma kwenye Mkutano wa Mwaka wa Jukwaa la Boao la Asia 2026

Eneo Jipya la Xiong'an la China labadilika kuwa mji wenye nguvu hai kutoka mpango
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma
