Binti mdogo afurahia maisha ya utotoni yenye furaha katika Mkoa wa Anhui, China (2)

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Juni 02, 2026
Binti mdogo afurahia maisha ya utotoni yenye furaha katika Mkoa wa Anhui, China
Maya (katikati) na wanafunzi wenzake wakishiriki kwenye shughuli ya Siku ya Watoto katika shule ya chekechea katika Mji mdogo wa Dongting wa Guangde, katika Mkoa wa Anhui, mashariki mwa China, Mei 29, 2026. (Picha na Jiang Wen/Xinhua)

Maya Ivanou mwenye umri wa miaka minne alihamia China na wazazi wake mwaka 2023. Familia hiyo inaishi katika Mji mdogo wa Dongting wa Mkoa wa Anhui, mashariki mwa China, ambapo ni Kituo kilipo cha Michezo ya Farasi cha kimataifa cha Delta ya Mto Changjjiang. Mama yake Maya, Aleksandra Timofeeva, anayejulikana zaidi kwa jina la Sasha, ni mcheza michezo ya farasi kutoka Russia na baba yake, Vasil Ivanou, ni kocha kutoka Belarus.

"Rafiki alipendekeza kazi kwa ajili yetu hapa klabuni. Kwa kuwa niliwahi kuishi China hapo awali na nilihisi vizuri kuhusu hali nchini China, hivyo familia yetu nzima iliamua kuja hapa," Sasha amesema.

Maya sasa anafurahia maisha ya utotoni yenye furaha nchini China. Katika chekechea, amejifunza Kichina na kujenga urafiki na watoto wenyeji.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha