Lugha Nyingine
Binti mdogo afurahia maisha ya utotoni yenye furaha katika Mkoa wa Anhui, China (6)
![]() |
| Maya akitembea na baba yake kwenye shamba la chai la Mji mdogo wa Dongting wa Guangde, katika Mkoa wa Anhui, mashariki mwa China, Januari 29, 2026. (Xinhua/Zhang Duan) |
Maya Ivanou mwenye umri wa miaka minne alihamia China na wazazi wake mwaka 2023. Familia hiyo inaishi katika Mji mdogo wa Dongting wa Mkoa wa Anhui, mashariki mwa China, ambapo ni Kituo kilipo cha Michezo ya Farasi cha kimataifa cha Delta ya Mto Changjjiang. Mama yake Maya, Aleksandra Timofeeva, anayejulikana zaidi kwa jina la Sasha, ni mcheza michezo ya farasi kutoka Russia na baba yake, Vasil Ivanou, ni kocha kutoka Belarus.
"Rafiki alipendekeza kazi kwa ajili yetu hapa klabuni. Kwa kuwa niliwahi kuishi China hapo awali na nilihisi vizuri kuhusu hali nchini China, hivyo familia yetu nzima iliamua kuja hapa," Sasha amesema.
Maya sasa anafurahia maisha ya utotoni yenye furaha nchini China. Katika chekechea, amejifunza Kichina na kujenga urafiki na watoto wenyeji.
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma




