Trump asema Marekani inakaribisha matarajio ya mazungumzo ya moja kwa moja kati ya Zelensky na Putin

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Juni 05, 2026

WASHINGTON - Rais wa Marekani Donald Trump amesema kwamba Washington inakaribisha matarajio ya mazungumzo ya moja kwa moja kati ya Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky na Rais wa Russia Vladimir Putin, akiwataka kuafikiana ili kumaliza mgogoro huo uliodumu kwa miaka mingi.

"Ninafurahi kwamba labda wanazungumzia kuhusu kukutana," Trump amewaambia waandishi wa habari jana Alhamisi katika Ikulu ya White House, akijibu barua ya wazi ambayo ndani yake Zelensky amependekeza mazungumzo ya moja kwa moja na Putin. "Nadhani itakuwa vizuri kama watakutana. Wanapaswa kukutana. Maliza hilo."

"Wote wawili wataafikiana, nilipendekeza maafikiano hayo, na ... tumekuwa na mengi yanayohusu nayo," Trump amesema.

Trump alikataa kuweka wazi ni mambo gani hayo ya maafikiano ambayo viongozi hao walikubaliana kufanya ili kukomesha mgogoro huo.

Mapema Alhamisi, Zelensky alitoa wito kwa Putin kushiriki katika mazungumzo ya moja kwa moja ili kumaliza vita, akijenga hoja kwamba mapigano yanayoendelea yanaathiri rasilimali za Russia na nafasi yake ya kimataifa.

"Ukraine inapendekeza kumaliza vita hivi kupitia ushiriki wa moja kwa moja kati yetu -- na wewe. Ninapendekeza mkutano," alisema katika barua ya wazi iliyochapishwa kwenye tovuti ya rais wa Ukraine.

Msemaji wa Kremlin Dmitry Peskov amesema jana Alhamisi kuwa Zelensky anaweza kuja Moscow wakati wowote kama akitaka kufanya mazungumzo.

"Rais Putin alisema kwamba kama Zelensky akitaka kuzungumza, anaweza kuja Moscow na kufanya hivyo," Peskov amesema.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha