Rais wa Afrika Kusini atangaza mpango wa kukabiliana na uhamiaji haramu

(CRI Online) Juni 08, 2026

Rais Cyril Ramaphosa wa Afrika Kusini ametangaza mfululizo wa hatua zinazolenga kukabiliana na uhamiaji haramu kufuatia wasiwasi unaoongezeka wa umma juu ya suala hilo.

Akihutubia taifa jana Jumapili mjini Pretoria, Rais Ramaphosa amesema baraza la mawaziri limepitisha mbinu za kina za usimamizi wa uhamiaji, zinazolenga kuimarisha utekelezaji wa shughuli za uhamiaji, kuhakikisha usalama wa mipaka, kupambana na ufisadi, na kuboresha mfumo na sera za uhamiaji.

Amesema chini ya mbinu hizo mpya, serikali itaongeza juhudi za kuwatambua na kuwarejesha nyumbani wahamiaji wasio na utambulisho rasmi, kuanzisha mahakama maalumu za uhamiaji ili kuharakisha mchakato wa kuwarejesha nyumbani wahamiaji hao, kuimarisha usalama wa mipaka, na kuweka faini kali zaidi kwa waajiri ambao wanaajiri wageni wasio na utambulisho rasmi kwa makusudi.

(Wahariri wa tovuti:Zhao Jian)

Picha