Rwanda yajitayarisha kukabiliana na mlipuko wa Ebola unaoweza kutokea

(CRI Online) Juni 08, 2026

Waziri Mkuu wa Rwanda Justin Nsengiyumva amesema, nchi hiyo imeweka hatua za kuzuia, ufuatiliaji na matibabu ili kukabiliana na mlipuko wowote wa Ebola unaoweza kutokea nchini humo, huku ikilinda afya ya umma na shughuli za kiuchumi.

Bw. Nsengiyumva amesema hayo Jumamosi iliyopita wakati akitoa taarifa kwa wanahabari huko Kigali, mji mkuu wa Rwanda.

Amesema, wana uhakika kwamba wana vifaa vya kulinda maisha ya raia bila ya kuvuruga shughuli za kijamii na kiuchumi, huku akitoa wito kwa wakazi kuwa na tahadhari, kuhakikisha usafi na kumripoti mtu yeyote wanayemshuku.

Akizungumza katika mkutano huohuo na wanahabari, waziri wa afya wa nchi hiyo Bw. Sabin Nsanzimana ameeleza kuwa nchi hiyo imejenga uwezo katika nyanja tano, zikiwemo za mawasiliano, ufuatiliaji, uwezo wa utambuzi, uwezo wa kufuatilia watu waliokutana na watu wanaoshukiwa kuambukizwa na usimamizi wa wagonjwa kwa kupitia vituo vya matibabu vilivyozinduliwa.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha