Vituo vya reli kwenye Uwanda wa Juu vyaleta urahisi kwa wakazi Mkoani Xizang (2)

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Juni 12, 2026
Vituo vya reli kwenye Uwanda wa Juu vyaleta urahisi kwa wakazi Mkoani Xizang
Sangye Phuntsok, mfanyakazi wa kituo cha reli ya Yanshiping, akizungumza na abiria kwenye kituo hiki katika Wilaya ya Amdo ya Nagqu, Mkoa unaojiendesha wa Xizang, kusini magharibi mwa China, Juni 11, 2026. (Xinhua/Tenzing Nima Qadhup)

LHASA – Kituo cha reli ya Yanshiping kiko katika Wilaya ya Amdo ya Nagqu, ambayo ni sehemu ya mwinuko wa mita 4,721 kutoka juu ya bahari katika Mkoa unaojiendesha wa Xizang, kusini-magharibi mwa China, kituo hicho ni moja ya vituo vya reli vilivyoko kwenye sehemu za mwinuko wa juu zaidi duniani. Kituo hicho kilichojengwa Tarehe Mosi, Julai, 2006, hapo awali kilikuwa kituo kisicho na wahudumu kilichotumika tu kwa treni kutua kwa muda, na kilianza kuwa kituo cha kudumu cha reli chenye ratiba maalum mwezi Desemba 2025, na hivyo kimeleta urahisi zaidi kwa wakazi wa huko.

(Wahariri wa tovuti:Liu Mengxue,Zhao Jian)

Picha