Mkoa wa Fujian wajitokeza ukiwa kitovu kikuu muhimu cha nishati safi kusini mwa China (3)

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Julai 10, 2026
Mkoa wa Fujian wajitokeza ukiwa kitovu kikuu muhimu cha nishati safi kusini mwa China
Picha iliyopigwa Julai 7, 2026 ikionyesha eneo la ujenzi wa sehemu ya No. 3 ya mashine za mradi wa nishati ya nyuklia wa Zhangzhou katika Wilaya ya Yunxiao, Mkoa wa Fujian, kusini mashariki mwa China. (Xinhua/Lin Shanchuan)

Mkoa wa Fujian ulioko kusini mashariki mwa China una utajiri wa rasilimali za nishati safi zenye sifa bora kama vile nishati ya upepo, nishati ya jua, nishati ya maji na nishati ya nyuklia.

Katika miaka ya hivi karibuni, mkoa wa Fujian ukitegemea nguvu bora yake ya nishati safi na hali ya kijiografia umejenga gridi zake mpya za kisasa za umeme na kuundeleza mkoa huo kuwa kituo muhimu cha nishati safi kusini mashariki mwa China.

Mkoa huo umeharakisha ujenzi wa njia za kusambaza umeme, umeboresha mitandao ya kusambaza umeme mijini na vijijini kwa hatua madhubuti, umehimiza ujenzi wa gridi ndogo ndogo za umeme za kisasa, umehuisha nguvu zake bora za nishati safi hatua kwa hatua, na kuimarisha msingi wa usalama wa nishati kwa kupitia ujenzi wa gridi mpya za kisasa za umeme.

(Wahariri wa tovuti:Liu Mengxue,Zhao Jian)

Picha