Ushoroba wa mashariki wa Reli ya China-Ulaya waongeza ushirikiano wa kiwango cha juu wa BRI

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Julai 15, 2026
Ushoroba wa mashariki wa Reli ya China-Ulaya waongeza ushirikiano wa kiwango cha juu wa BRI
Picha iliyopigwa Julai 13, 2026 ikionyesha treni ya mizigo inayotoa huduma kati ya China na Ulaya ikifanyiwa mchakato wa kuhamishiwa kwa mzigo melini kwenye Stesheni ya Manzhouli katika Mji wa Manzhouli, Mkoa wa Mongolia ya Ndani, Kaskazini mwa China. (Picha na Huang Xu/Xinhua)

Kampuni ya Kundi la Reli la China la Harbin imesukuma mbele maendeleo ya mifumo ya kidijitali ya bandari na huduma za usafirishaji bidhaa kwa haraka kwenye reli wakati huohuo limekuwa likiboresha hatua kwa hatua hali ya kuunganishwa kwa miundombinu ya bandarini.

Jitihada hizo zimeongeza ufanisi na uwezo wa ushoroba wa mashariki wa huduma ya treni za mizigo kati ya China na Ulaya. Hadi kufikia Juni 2026, idadi ya jumla ya safari za treni za usafirishaji mzigo kwa haraka kwenye Reli ya China-Ulaya kupitia ushoroba huo wa mashariki ilikuwa imezidi 40,000.

Ushoroba huo wa mashariki, unaohusisha bandari tatu kuu za reli za Manzhouli, Suifenhe na Tongjiang, hadi sasa umeunganisha miji zaidi ya 60 ya China na nchi 14 za Ulaya kupitia njia 27 zenye ratiba maalum, na kuwa mfano wazi wa juhudi za kuhimiza ushirikiano wa kiwango cha juu wa Ukanda Mmoja, Njia Moja.

(Wahariri wa tovuti:Liu Mengxue,Zhao Jian)

Picha